
Habari juu ya tukio hilo linasema kwamba wasichana wawili walikuwa wanapiga picha na Chris Brown na wakati huohuo jamaa huyo alijaribu kwenda kwa nyuma na kuharibu picha hiyo (Photoboom). Chris Brown alivyomuona ndio hasira zake zikamfanya amrushie ngumi ya uso na kumpata puani.
Watu wakaribu na Chris Brown wametoa habari tofauti juu ya tukio hili na kusema kwamba huyo jamaa alikuwa anajaribu kupanda tour bus la Chris Brown lakini alizuiwa. Jamaa huyoalitaka kupanda baada ya wasichana wengine kukataliwa sasa katika harakati za kuzuiwa asiingine ndio aliumia puani.
No comments:
Post a Comment