Social Icons

Sunday 25 May 2014

Baada ya Mechi ya Jana UEFA Kocha wa Spain,Vincente Del Bosque atangaza kikosi cha wachezaji 29 wengine watemwa


Kocha wa Mabingwa wa Dunia Spain,Vincente Del Bosque, amechelewesha kutaja Kkosi chake cha mwisho cha Wachezaji 23 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil na badala yake amemwita Gerard Deulofeu, aliekuwa Everton kwa Mkopo, na kuwaacha Wachezaji wa Real Madrid na Atletico Madrid kwa ajili ya Mechi ya kujipima nguvu na Bolivia.
Ilitegemewa kuwa Leo hii Vincente Del Bosque angelipunguza Kikosi chake kutoka Wachezaji 30 na kubakisha 23 tu kama inavyotakiwa na FIFA kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia lakini badala yake amewaita Wachezaji 19 tu kwa ajili ya Mechi ya Ijumaa Mei 30 na Bolivia.

Wachezaji wote wa Real na Atletico waliokuwemo kwenye Kikosi cha Awali cha Wachezaji 30 hawakuitwa kwa ajili ya Mechi na Bolivia na Vincente Del Bosque amesema: “Hatuhitajiki kuwapa FIFA Listi ya Wachezaji 23 hadi Juni 2, sasa kwa nini tutangaze sasa?”Uamuzi huu utawanufaisha sana Wachezaji Majeruhi kama vile Diego Costa wa Atletico Madrid na kuwapa muda zaidi wa kupona.


Lakini Mchezaji alienufaika sana ni Kiungo wa Barceloana, Gerard Deulofeu, ambae Msimu huu alikuwa England kwa Mkopo huko Everton hasa kwa vile yeye si mmoja wa Wachezaji 30 waliotangazwa awali.Del Bosque ameeleza: “Tunamwamini na hasa Wachezaji wakijitoa Kikosini yeye anafaa tu!Wachezaji wengine waliokuwemo kwenye Kikosi cha Wachezaji 30 lakini wameachwa kwenye Mechi hii na Bolivia itakayochezwa huko Seville ni pamoja na Wachezaji wawili wa Man City, Jesus Navas na Alvaro Negredo, pamoja na Straika wa Juventus, Fernando Llorente. 

KIKOSI KILICHOITWA KUCHEZA NA BOLIVIA:
Pepe Reina, David De Gea, Gerard Pique, Raul Albiol, Javi Martinez, Jordi Alba, Cesar Azpilicueta, Alberto Moreno, Zavi Hernandez, Andres Iniesta, Sergio Busquets, Santi Cazorla, Ander Iturraspe, Cesc Fabregas, Juan Mata, David Silva, Pedro Rodriquez, Fernando Torres, Gerard Deulofeu.

No comments:

Post a Comment