Social Icons

Friday 16 May 2014

Jumamosi kesho Wembley Stadium Jijini London Fainali ya FA CUP Arsenal vs Hull City tazama Tathimini Hapa


Watu wengi huko Uingereza hii ni nafasi murua kwa Arsene Wenger na Arsenal yake kumaliza ukame wao wa Miaka 9 bila ya Kombe lolote wakati Jumamosi watakapoingia Wembley Stadium Jijini London kuivaa Hull City kwenye Fainali ya FA CUP.
Arsenal wanapambana na Hull City ambao wamemaliza Msimu huu wakiwa Nafasi ya 16 kwenye Ligi Kuu England lakini kwa Meneja wa Hull City, Steve Bruce, Nguli wa Man United, faraja kubwa ni kukumbuka nini kiliwakuta Arsenal Miaka mitatu iliyopita walipotinga Wembley kwenye Fainali ya Kombe la Ligi na kuchapwa 2-1, bila kutarajiwa, na Birmingham City.Wakiwa na Masupastaa kama kina Mesut Ozil, Santi Cazorla na Olivier Giroud, utabiri wote unanyoosha kidole kuwa Arsenal ndio Bingwa wa FA CUP na hasa ukizingatia Rekodi mbovu ya Hull City dhidi ya Arsenal ya kufungwa Mechi zote 2 za Ligi Kuu England Msimu huu na pia kutoifunga Arsenal tangu wakutane uso kwa uso kuanzia Mwaka 2009.

SAFARI KWENDA WEMBLEY
ARSENAL
Raundi ya 3
Arsenal 2 Tottenham 0
Raundi ya 4
Arsenal 4 Coventry 0
Raundi ya 5
Arsenal 2 Liverpool 1
Raundi ya 6
Jumamosi Machi 8
Arsenal 4 Everton 1
Nusu Fainali
Wigan 1 Arsenal 1
[Penati: Arsenal 4-2]

HULL CITY
Raundi ya 3
Middlesbrough 0 Hull City 2
Raundi ya 4
Southend 0 Hull City 2
Raundi ya 5
Brighton 1 Hull City 1
[Marudiano Hull 2 Brighton 1]
Raundi ya 6
Hull City 3 Sunderland 0
Nusu Fainali
Hull City 5 Sheffield United 3


Wenger anatarajiwa kufanya uamuzi nani amuweke Golini kati ya Kipa Lukas Fabianski, ambae amedaka Mechi zao zote za FA CUP Msimu huu, au Kipa Nambari Wani Wojciech Szczesny, ambae ametwaa Glovu za Dhahabu Msimu huu baada ya kuweka Rekodi ya kutofungwa katika Mechi 16 za Ligi Kuu England.
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
Arsenal: Fabianski; Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs; Ramsey, Arteta; Ozil, Cazorla, Podolski; Giroud
HULL CITY: Harper; Bruce, Chester, Davies, Figueroa, Rosenior; Livermore, Huddlestone, Elmohamady; Boyd; Sagbo
REFA: Lee Probert

No comments:

Post a Comment