Social Icons

Sunday 25 May 2014

Maoni yawapiga kura yanaonyesha kuwa Poroshenko atashinda kuwa rais Ukraine


Matokeo yanayotokana na maoni ya wapigaji kura yanaonesha kuwa biliyoneya anayetengeneza chakileti, Petro Poroshenko, ameshinda katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa rais wa Ukraine.
Inakisiwa amepata asili-mia 56 ya kura.Matokeo rasmi hayatotangazwa hadi Jumatatu.Bwana Poroshenko alisema azma yake ni "kumaliza vita na kuleta amani", na alisema Ukraine daima haitokubali Urusi "kulikalia" jimbo la Crimea.

Waziri Mkuu wa Urusi, Dmitri Medvedev, alizuru Crimea wakati upigaji kura unaendelea, hatua ambayo serikali ya Kiev imesema ni uchokozi wa kusudi.Upigaji kura ulisonga mbele ingawa vituo vya kupigia kura havikufunguliwa katika miji ya Mashariki ya Donetsk na Luhansk.

No comments:

Post a Comment