Social Icons

Monday 12 May 2014

Fainali za Kombe la Dunia RUSSIA, ALGERIA na GHANA,zimetangaza Vikosi vyao


NCHI 32 ambazo zitacheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil kuanzia Juni 12 zipo mbioni kutangaza na kuwasilisha Vikosi vyao vya Awali vya Wachezaji wasiozidi 30 kwa FIFA kabla ya Siku ya mwisho hapo Mei 13.Listi za mwisho za Wachezaji 23 kwa Timu hizo 32 zinapaswa kutua FIFA ifikapo Juni 2.


LEO HII RUSSIA, ALGERIA na GHANA,  zimetangaza Vikosi vyao.Awali Leo, Japan na England zilitaja Wachezaji wao.

RUSSIA YATAJA TIMU YA BRAZIL, PAVLYUCHENKO NJE!
MASTAA wa Klabu ya Lokomotiv Moscow, Roman Pavlyuchenko na Dmitry Tarasov, wameachwa kwenye Kikosi cha Russia cha Awali cha Wachezaji 30 waliotajwa na Kocha Fabio Capello ambae pia ameshangaza wengi kwa kumuita Straika Mkongwe Pavel Pogrebnyak, mwenye Miaka 30, ambae anacheza Daraja la Championship huko England na Klabu ya Reading.Russia wanatarajiwa kujipima nguvu na Slovakia hapo Mei 26, Norway Mei 31 na Morocco hapo Juni 6.Huko Brazil, Russia, ambao hii ni mara ya kwanza kucheza Fainali za Kombe la Dunia tangu Mwaka 2002, wapo KUNDI H pamoja na Belgium, South Korea na Algeria.

KIKOSI KAMILI:
MAKIPA:Igor Akinfeev (CSKA Moscow), Yury Lodygin (Zenit St Petersburg), Sergei Ryzhikov (Rubin Kazan)

MABEKI: Alexander Anyukov (Zenit St Petersburg), Alexei Berezutsky, Vasily Berezutsky, Sergei Ignashevich, Georgy Shchennikov (all CSKA Moscow), Vladimir Granat, Alexei Kozlov (both Dynamo Moscow), Andrei Yeshchenko (Anzhi Makhachkala), Dmitry Kombarov (Spartak Moscow), Andrei Semenov (Terek Grozny)
VIUNGO: Igor Denisov, Yury Zhirkov (both Dynamo Moscow), Alan Dzagoev (CSKA Moscow), Yury Gazinsky, Roman Shirokov (both FC Krasnodar), Denis Glushakov (Spartak Moscow), Pavel Mogilevets (Rubin Kazan), Viktor Faizulin, Oleg Shatov (both Zenit St Petersburg)

MAFOWADI: Vladimir Bystrov (Anzhi Makhachkala), Alexander Kerzhakov (Zenit St Petersburg), Artem Dzyuba (Rostov), Alexei Ionov, Alexander Kokorin (both Dynamo Moscow), Maxim Kanunnikov (Amkar Perm), Pavel Pogrebnyak (Reading/ENG), Alexander Samedov (Lokomotiv Moscow)

ALGERIA YATANGAZA 30
Algeria, chini ya Kocha Vahid Halilhodzic, imetangaza Kikosi chake cha Wachezaji 30 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil zinazoanza Juni 12 na wapo Wachezaji kadhaa wanaocheza huko England.
Chipukizi wa Tottenham Nabil Bentaleb na Kiungo wa Leicester City Riyad Mahrez, ambae ameitwa kwa mara ya kwanza, wanaungana na Rafik Djebbour wa Nottingham Forest kwenye Timu hiyo.Bentaleb aliingizwa Timu ya Kwanza ya Tottenham mara baada kuteuliwa Meneja Tim Sherwood na Mwezi Machi aliamua kuichezea Algeria kwa mara ya kwanza badala ya France alikozaliwa.Riyad Mahrez ameitwa kwa mara ya kwanza kuichezea Algeria na Kocha Vahid Halilhodzic amekiri kumwona Mchezaji huyo aliezaliwa France mara ya kwanza Mwezi Februari na kuvutiwa mno.Huko Brazil , Algeria wako KUNDI H pamoja na Belgium, Russia na South Korea.

KIKOSI KAMILI:
MAKIPA: Azzedine Doukha (USM El Harrach), Rais Mbolhi (CSKA Sofia), Cedric Si Mohamed (CS Constantine), Mohamed Lamine Zemmamouche (USM Alger)

MABEKI: Essaid Belkalem (Watford), Madjid Bougherra (Al Lekhwiya), Liassine Cadamuro (Mallorca), Faouzi Ghoulam (Naples), Rafik Halliche (Academica Coimbra), Nacereddine Khoualed (USM Alger), Aissa Mandi (Stade Reims), Carl Medjani (Valenciennes), Djamel Mesbah (Livorno), Mehdi Mostefa (Ajaccio)

VIUNGO: Nabil Bentaleb (Tottenham Hotspur), Ryad Boudebouz (Bastia), Yacine Brahimi (Granada), Abdelmoumene Djabou (Club Africain), Sofiane Feghouli (Valencia), Adlene Guedioura (Crystal Palace), Foued Kadir (Stade Rennes), Amir Karaoui (Entente Setif), Mehdi Lacen (Getafe), Riyad Mahrez (Leicester City), Saphir Taider (Inter Milan), Hassan Yebda (Udinese)

MAFOWADI: Rafik Djebbour (Nottingham Forest), Nabil Ghilas (Porto), Islam Slimani (Sporting), El Arabi Soudani (Dinamo Zagreb).

GHANA YATANGAZA 26!
Ghana, chini ya Kocha Akwasi Appiah, imetaja Kikosi chake cha Awali cha Kombe la Dunia na wamo Magwiji wao wote kina Michael Essien na Sulley Muntari wa AC Milan, Kevin Prince-Boateng wa Schalke na Asamoah Gyan anaecheza Al Ain ya Falme za Nchi za Kiarabu.
Ghana watacheza Mechi ya Kirafiki na Holland hapo Mei 31 na baadae kupunguza Kikosi hicho kufikia Wachezaji 23.

MAKIPA: Stephen Adams (Aduana Stars), Fatau Dauda (Orlando Pirates), Adam Kwarasey (Stromsgodset)

MABEKI: Harrison Afful (Esperance), Jerry Akaminko (Eskisehirspor), John Boye (Stade Rennes), Samuel Inkoom (Platanias), Jonathan Mensah (Evian Thonon Gaillard), Daniel Opare (Standard Liege), Jeffrey Schluup (Leicester City), Rashid Sumaila (Mamelodi Sundowns)

VIUNGO: David Accam (Helsingborg), Afriyie Acquah (Parma), Albert Adomah (Middlesbrough), Emmanuel Agyemang Badu (Udinese), Kwadwo Asamoah (Juventus), Christian Atsu (Vitesse Arnhem), Andre Ayew (Olympique Marseille), Michael Essien (AC Milan), Rabiu Mohammed (Kuban Krasnodar), Sulley Muntari (AC Milan), Mubarak Wakaso (Rubin Kazan)

MAFOWADI: Jordan Ayew (Sochaux), Kevin Prince Boateng (Schalke 04), Asamoah Gyan (Al Ain), Abdul Majeed Waris (Valenciennes).

No comments:

Post a Comment