Social Icons

Friday 6 June 2014

Alex Oxlade-Chamberlain Hatarini Kushiriki Fainali za Kombe la Dunia


Kushiriki kwa Alex Oxlade-Chamberlain kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Nchini Brazil Alhamisi Juni 12 kupo kwenye hati hati kubwa baada ya Kiungo huyo wa Arsenal kuumia Goti kwenye Mechi ya Jumatano Usiku ambayo England walitoka 2-2 na Ecuador huko Miami, Marekani.
Oxlade-Chamberlain, mwenye Miaka 20, anaendelea kutibiwa na kuchunguzwa na Madaktari wa England lakini habari za awali zimedai kuwa anahitaji Siku 10 hadi Wiki 3 ili apone.Ingawa Juni 2 ndio ilikuwa Siku ya mwisho kwa Timu zote 32 zilizopo Fainali za Kombe la Dunia kuwasilisha Listi yao ya Wachezaji 23, lakini Timu zinaweza kubadili Mchezaji hadi Juni 13 ikiwa FIFA itaridhishwa kuwa mabadiliko hayo ni kwa ajili ya Majeruhi tu.


WACHEZAJI 7 WA AKIBA:
-John Ruddy (Norwich)
-John Flanagan (Liverpool),
-John Stones (Everton),
-Michael Carrick (Man Utd),
-Jermain Defoe (Toronto),
-Andy Carroll (West Ham),
-Tom Cleverley (Man Utd).

Kocha wa England, Roy Hodgson, amekiri: “Itakuwa pigo kubwa kumkosa. Alifanya vizuri sana kwenye Mechi na alionekana kuwa mwepesi mno!”Mechi hiyo na Ecuador ilikuwa ni Mechi ya kwanza ya Oxlade-Chamberlain tangu Aprili 20 alipoumia Nyonga akiwa na Klabu yake Arsenal.jana, Oxlade-Chamberlain alikuwepo Mazoezini huko Kambini kwa England, Barry University, Miami, akifanya Mazoezi mapesi huku akiwa na Bendeji Gotini.

No comments:

Post a Comment