Social Icons

Thursday 26 June 2014

FIFA Yamfungia Ng'atang'ata (Luis Suarez) Miezi 4 Na Mechi Tisa


Straika wa Uruguay Luis Suarez amefungiwa Miezi Minne kutoshiriki chochote kwenye Soka baada ya kupatikana hatia ya kumuuma Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini.Straika huyo wa Liverpool pia amefungiwa Mechi 9 za Kimataifa zitakazomfanya awe nje ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.


Adhabu hii pia inamaanisha atazikosa Mechi 9 za kwanza za Klabu yake Liverpool za Ligi Kuu England kwa Msimu mpya Tukio hili la kumng’ata Meno Chiellini lilitokea Juzi Jumanne kwenye Mechi ya mwisho ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia ambayo Uruguay iliifunga Italy 1-0 na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano.

FIFA imetamka haitazungumza lolote kuhusu Kesi ya Luis Suarez anaetuhumiwa kumng’’ata Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini hadi Kamati ya Nidhamu imalize shauri lake lakini Wadau na Malejendari wa Klabu ya Liverpool wamezungumza kwamba Mchezaji huyo ameiaibisha na kuifedhehesha Klabu yake hiyo.

Suarez alionekana akimng’ata Meno Chiellini kwenye Mechi ya mwisho ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia ambayo Nchi yake Uruguay iliifunga Italy Bao 1-0 na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano.Refa Marco Rodriguez wa Mexico, ambae huko kwao amebatizwa Jina ‘Dracula’ kwa ukali wake Uwanjani, hakuona tukio hilo na licha ya Chiellini kumwonyesha alama za Meno hakuchukua hatua yeyote. 


Hata hivyo Kanuni za FIFA zinaruhusu Mchezaji kuhukumiwa kwa ushahidi wa Video hata kama Refa aliliona tukio na kutochukua hatua.Suarez amepewa hadi Usiku wa Leo Saa 5 Usiku, Saa za Bongo, kujibu tuhuma hizo ambazo akipatikana na hatia FIFA inao uwezo wa kumfungia Mechi 24 au Miaka miwili kote Duniani kwa Mechi za Ndani, za Klabu, na za Kimataifa. 

Akizungumzia Shauri hilo, Msemaji wa FIFA Bibi Delia Fischer amesema: “Uchunguzi unaendelea na bado ni mapema. Hatuwezi kuzungumza nini kitatokea hilo lipo mikononi mwa Kamati ya Nidhamu. Tutatoa tamko baadae Leo au Kesho mara tu wakiamua.”

Kifungo cha juu kabisa kumkumba Mchezaji kwa kosa wakati wa Fainali za Kombe la Dunia ni kile cha Mwaka 1994 kwa Mchezaji wa Italy, Mauro Tassotti, cha Mechi 8 baada kumvunja Pua kwa kiwiko Mchezaji wa Spain, Luis Enrique, ambae sasa ni Meneja mpya wa Barcelona.

Malejendari Liverpool
Wakati huo huo, Malejendari wa Liverpool, Phil Thompson na Robbie Fowler, wamezungumzia tukio la hivi sasa la Luis Suarez na kudai Mchezaji huyo ameiaibisha na kuifedhehesha Klabu yake Liverpool.

Phil Thompson, Nahodha wa zamani na Meneja Msaidizi wa Liverpool, amesema: “Nilivunjika nguvu kabisa nilipoona picha zile na kutaka hilo lisingetokea tena. Huyu ni Mchezaji Bora wa England, anaichezea Klabu yangu na ameleta aibu, ameleta fedheha klabuni!”
Nae Mchezaji wa zamani wa Liverpool, Robbie Fowler, amesema Suarez ameipaka matope Liverpool.

Hii si mara ya kwanza kwa Suarez kung’ata Meno Mpirani kwani Aprili 2013, Luis Suarez alifungiwa Mechi 10 kwa kumuuma Meno Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.Mwaka 2010 huko Uholanzi, Suarez alifungiwa Mechi 7 kwa kumuuma Kiungo wa PSV Eindhoven Otman Bakkal. 

Wachambuzi wengi huko England wanahisi tukio hili litamng’oa Liverpool na kutokomea huko Spain kujiunga na Real Madrid au Barcelona kama mwenyewe alivyokuwa akitaka tangu Msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment