Social Icons

Friday 13 June 2014

Afrika Yaanza kwa Kutereza Kombe la Dunia Mexico yailaza Cameroon bao 1-0.


Mexico yajikita katika nafasi ya pili ya Kundi A nyuma ya Brazil baada ya ushindi wa bao moja kwa nunge dhidi ya wawakilishi wa Afrika the Indomitable lions ya Cameroon.Mechi hiyo ndiyo iliyokuwa ya pili baada ya ushindi tata wa Brazil dhidi ya Craotia hapo jana.


Kama mechi hiyo ya ufunguzi iliyoshuhudia maamuzi tata, Mabao mawili ya mshambulizi wa Giovanni Dos Santos yalifutiliwa mbali kutokana na kile wachambuzi wa mechi waliashiria kuwa ni makosa ya naibu wa refarii.

Licha ya hayo Mkwaju wa Dos Santos ulipanguliwa na kipa wa Cameroon kabla ya Oribe Peralta kufuma bao hilo la pekee na la ushindi kunako dakika ya 61 ya kipindi cha pili.Mexico sasa inatoshana nguvu na Brazil kileleni mwa kundi A.

No comments:

Post a Comment