Social Icons

Sunday 22 June 2014

Ronaldo Ampongeza Klose Kuifikia Rekodi Yake Kombe la Dunia , Dzeko Amlaumu Refa Kutupwa Nje Bosnia


Straika wa zamani wa Brazil Ronaldo amempongeza Miroslav Klose baada ya Mjerumani huyo kuifikia Rekodi yake ya Bao 15 za kwenye Fainali za Kombe la Dunia.
Klose, Miaka 36, alitokea Benchi kwenye Mechi ya Jana ya Kombe la Dunia huko Brazil na kuisawazishia Germany walipotoka Sare ya 2-2 na Ghana kwenye Mechi ya Kundi G.


Akiposti kwenye Mtandao wa Twitter, Ronaldo alisema: “Karibu kwenye Klabu. Naifikiria furaha yako. Hili ni Kombe la Dunia bora!”Ronaldo alifunga Goli zake hizo 15 kwenye Fainali za Kombe la Dunia za 1998, 2002 na 2006.  



Klose amepia Bao kwenye Fainali za Kombe la Dunia za 2002, Bao 5, zote za Kichwa, Mwaka 2006 Bao 5 na Mwaka 2010 Bao 4.


Vile vile Klose ameifikia Rekodi ya Lejendari wa Brazil Pele na Mjerumani, Uwe Seeler, ya kufunga Bao katikaFainali za Kombe la Dunia 4 mfululizo.



DZEKO AMLAUMU REFA KWA BOSNIA KUTUPWA NJE YA KOMBE LA DUNIA


Bosnia-Hercegovina walitupwa nje ya Fainali za Kombe la Dunia hapo Jana Jumamosi huko Cuiaba, Brazil baada kufungwa Bao 1-0 na Nigeria lakini Straika wao, Eden Dzeko, amemlaumu Refa kwa kushindwa kwao.

Kwenye Mechi hiyo ya Kundi F, Dzeko alifunga Bao safi Kipindi cha Kwanza lakini Refa Peter O´Leary wa New Zealand alilikataa Bao hilo kwa madai ni Ofsaidi lakini marudio yalionyesha Straika huyo wa Manchester City hakuwa Ofsaidi.Nigeria walishinda kwa Bao 1-0 lililofungwa na Peter Odemwingie anaechezea Stoke City huko England. 

Bosnia walifungwa Bao 2-1 na Argentina kwenye Mechi ya Kwanza na hivyo kubakisha Mechi moja ya kukamilisha Ratiba na Iran huku Nigeria wakicheza na Argentina na kuhitaji Sare au hata kufungwa ikiwa Iran haitaifunga Bosnia.



Akiongea kwa hasira baada ya Mechi ya Jana, Dzeko, ambae alidai mbali ya kukataa Bao lao safi hata Bao la Nigeria lilitokea baada ya Emmanuel Emenike kumchezea Rafu Emir Spahic kabla hajampasia Mfungaji Odemwingie.

Dzeko alifoka: “Tunarudi nyumbani, tuna huzuni na Refa pia anastahili kurudi nyumbani kwa sababu alibadilisha matokeo na ndio maana tumefungwa!”

No comments:

Post a Comment